Dodoma; Tarehe 30 Mei, 2025;
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepongezwa na kuhimizwa kuendeleza ushirikiano na wadau wa sektambalimbali za kiuchumi na Kijamii ili kuongeza uelewa wamatumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa pamoja na ufanisikatika uzingatiaji wa sheria Namba 2 ya mwaka 2019 ya mamlaka ya hali ya hewa Tanzania.
Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Hali yahewa Tanzania(NMTC) Dkt, Emmanuel Mpeta KatikaUfunguzi wa warsha ya uelewa wa huduma za hali ya hewa, zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwawadau kuitoka sekta mbalimbali nchini, wakiwemoWanahabari. Mafunzo haya yalifanyika kuanzia Tarehe 27 – 30, Mei 2025 kwenye ukumbi wa Royal village jijiniDodoma.
“Nawapongeza TMA kwa kuendelea kuwashirikisha wadauwa sekta mbalimbali kw lengo la kuimarisha matumizi yataarifa ya za hali ya hewa katika shughuli za kijamii nakiuchumi. Warsha hii ni fursa muhimu ya kuboresha hudumaza hali ya hewa na kuimarisha matumizi sahihi ya huduma zahali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya HewaTanzania, ikiwemo uzingatiaji wa Sheria ya Mamlaka ya Haliya Hewa Na.2 ya 2019 katika shughuli zinazotumia au zinazotakiwa kutumia huduma za hali ya hewa nchini. Warshahii pia ni fursa ya kujenga na kuimarisha uelewa kuhusiana nachangamoto na fursa za mabadiliko ya hali ya hewa na Tabianchi.” alisema Dkt. Mpeta
Dkt Mpeta alisisitiza pia umuhimu wa wadau wote kuzingatiasheria Na 2 ya Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania katikashughuli zao za kila siku za kiuchumi na kijamii. “Utekelezajiwa sheria ya Mamlaka unaambatana na jukumu la kusimamiahuduma za hali ya hewa pamoja na udhibiti wa shughuli zahali ya hewa hapa nchini. Mkutano huu ni muhimu katikakuwajengea wadau uelewa wa nini wanapaswa kufanya kwamujibu wa Sheria”.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Mabadiliko yaTabianchi Dkt, Ladislaus Chang’a aliwashukuru wafadhili waMradi wa “WISER” na washirika wengine kwa kuendeleakushirikiana na TMA katika kuimarisha huduma za hali yahewa.
Aidha, Dkt. Chang’a alisisitiza umuhimu wa kuzingatiamatumizi sahihi ya huduma za hali ya hewa katika kufanyamaamuzi stahiki wakati wote. Vilevile aliendelea kuvishukuruvyombo vya habari kwa kuendelea kuwa kiungo cha kutoahabari sahihi za hali ya hewa kwa jamii.
Warsha hii imehusisha wadau kutoka sekta mbalimbali zakiuchumi na kijamii nchini kama vile nishati, kilimo, maji, habari, maafa, Serikali za Mitaa pamoja na Sekta binafsi. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaendelea na juhudi zakuhakikisha jamii inapata uelewa mpana wa taarifa za hali yahewa kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa matumizi ya taarifa hizi kwenye shughuli za kiuchumi na kijamii.